
Akizungumza katika sherehe hiyo, Rais Magufuli amempongeza Rais Kenyatta na serikali yake kwa kujenga barabara hiyo ambapo amesema haitawasaidia wananchi wa Kenya tu, bali pia itawasaidia wananchi wa Afrika Mashariki wanaotumia barabara zinazopitia Nairobi.
“Wananchi wanahitaji maendeleo na haya ndio maendeleo, barabara hii itasaidia kuinua uchumi na itasaidia masuala ya kijamii,” alisema Rais Magufuli.
Barabara hiyo ina urefu wa kilometa 28 na inaunganisha maeneo mbalimbali ya jiji la Nairobi. Uzinduzu huo umefanyika katika eneo la Karen nje kidogo ya jiji la Nairobi.
Hizi ni baadhi ya picha katika ufunguzi wa barabara hiyo:


No comments:
Post a Comment